Skip to main content

John Cena Achukua Nafasi ya Finn Balor , Sasa Kupambana Na Roman Reigns Agosti 21

Mkongwe wa WWE John Cena usiku wa Jana alirejea tena Kwenye kampuni hiyo Baada ya kukaa Nje ya mchezo Huo kwa Muda wa mwaka mmoja na nusu , Kurudi kwake kumeifanya WWE kurejea kwa Kishindo huku John akikiri kwamba Amerejea katika Mchezo huo kuuchukua Utawala wa Mashindano hayo Makubwa nchini Marekani.



Baada ya tukio hilo Sasa Bingwa wa WWE Universal Champion Roman Reigns atakabiliana na John Cena hii ni baada ya John kusaini mkataba wa Kupambana na Mpinzani huyo mnamo Agosti 21.


Awali Roman Reigns aligoma Kupigana na John Cena kwenye kipindi cha Smack Down wiki iliyopita na  kukubali kupambana na Mpinzani mwingine Finn Balor kisha John Cena akatokea na Kuchukua nafasi ya Finn hivyo Mpambano rasmi utakuwa Agosti 21 mwaka 2021.




Comments