Skip to main content

Posts

POPULAR POST

Zuchu Afikia Rikodi Hii Instagram , Awatibua Mastaa Wa Kike Bongo

Zuhura Othman anayetambulika kwa jina lake la kisanaa kama Zuchu anazidi kupanda nafasi kila kukicha baada ya kufikisha wafuasi milioni 5 katika mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo sasa anakaribia kuwafikia wafuasi wa msanii mwenzake Nandy ambaye ana wafuasi milioni 6.6 katika mtandao huo. Juma lililopita Zuchu alichapisha chapisho katika ukurasa wake wa instagram na kuwataka mashabiki zake kutomfanisha na msanii yoyote wa kike kutokea ukanda wa Afrika Mashariki na kudai kuwa kwa hatua aliyofika anapaswa kupambanishwa na wasanii wa kiume kwani anao uwezo mkubwa wa kuandika nyimbo na kutunga. “ Niwashukuru Wazazi wangu ni kwa ajili yenu na Uwezo wa m/mungu tu .kwa uandishi wangu yafaa kuwekwa kwenye ligi za wanaume wadada wenzangu ntawaonea tu. Respectfully my pen game hard I could write for a guy and not notice. Releasing two songs this month ,” - Zuchu. Zuchu ambaye anatamba na nyimbo zake mbili mpya alizoziachia hivi karibuni " Jaro " na " Fire " ndiye msanii ...
Recent posts

Erik ten Hag Asisitiza kuwa Ronaldo Hauzwi Manchester United

Kocha Mkuu wa Manchester United, Erik Ten Hag amesema mchezaji wa klabu hiyo na taifa la Ureno nyota Cristiano Ronaldo hatouzwa kwa sababu klabu hiyo ina malengo naye kwa ajili ya msimu ujao. Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na tetesi za kuwa Ronaldo anahitaji kuondoka United. Ten Hag ameongeza kuwa “Niliongea na Ronaldo kabla ya haya mambo kujitokeza na maongezi yetu yalikuwa mazuri na niko na mpango naye wa kumtumia tunataka kupate mafanikio tukiwa naye, kama nilivyosema mwanzo Ronaldo hauzwi” Aidha Erik ten Hag amethibitisha kuwa Harry Maguire atasalia kama nahodha wa Manchester United kwa msimu ujao na haoni kumbakiza nahodha kama suala muhimu. Huku United wakimwinda Lisandro Martinez msimu huu wa joto, Maguire atakabiliwa na ushindani zaidi katika nafasi yake na kumekuwa na uvumi kwamba Ten Hag anaweza kuteua nahodha mpya , Lakini Ten Hag amemuunga mkono Maguire kubaki na kitambaa hicho msimu huu. “Harry Maguire ndiye nahodha. Ni lazima niwafahamu wachezaji wote, lakini ni nahod...

Jux Akutana na Boss wa Hennessy , Apewa zawadi Yenye thamani ya EURO 3100

Msanii wa muziki wa RnB Juma Jux kutokea kiwanda cha muziki wa Bongo fleva ameendelea kutanua wigo wa biashara zake Kimataifa ambapo siku ya jana ameingia kwenye headlines kwa mara nyingine baada ya kuchapisha video katika ukurasa wake wa Instagram ikimuonesha akiwa kwenye mualiko wa chakula cha jioni na Boss na mwanafamilia waanzilishi wa Hennessy, bwana Maurice R. Hennessy. Kwenye mualiko huo, Jux pia amepewa zawadi ya chupa ya Hennessy iliyoandikwa jina lake, inayokadiriwa kuwa na thamani ya Euro 3,100 ambazo ni zaidi ya Shillingi Milioni 7.5 kwa fedha za hapa nyumbani. African Boy anameeleza kuwa safari zake nje ya nchi zitakwenda kufungua fursa nyingi za kibiashara kwake na vijana wengi hapa nchini.

Burna boy Aweka Rikodi mpya Africa , Aingiza Dola $7,276,150 kwa Usiku mmoja

Nyota wa muziki kutokea nchini Nigeria African Giant , Burna Boy ameingiza mabilioni ya fedha kutoka kwenye tamasha alilolifanya siku chache zilizopita Madison Square Garden , New York. Damini Ogulu, anayejulikana kwa jina lake la kisanaa kama Burna Boy, amekuwa msanii wa kwanza wa muziki wa Nigeria kufikia rikodi hiyo ambapo Odogwu amejinyakulia zaidi ya bilioni N3 za mauzo ya tiketi pekee. Tiketi ziliuzwa kwa bei ya chini kwa dola $80 na wastani wa dola $350 huku tiketi za juu Zikiuzwa kwa dola $2,125. Kulingana na hesabu za Business Day kwa kutumia wastani wa mauzo ya N145,365.50 ambapo ni dola ($350) ikizidishwa na jumla ya uwezo kuchukua watazamaji unaopatikana katika uwanja wa huo 20,789, na kiwango cha ubadilishaji cha sasa cha fedha za kigeni nchini Nigeria N415.33 jumla yake ni $7,276,150 ambayo ni zaidi ya N3,03022,090. . Tamasha hilo la kihistoria lililotumia takribani saa 2 liliruka moja kwa moja kwenye Youtube na kupata watazamaji zaidi ya 81,000 mashabiki kutoka nc...

Mtoto wa Kiume wa Cristiano Ronaldo Afariki Usiku wa Jana

Mshambuliaji wa Manchester United raia wa Ureno , Cristiano Ronaldo kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii ametangaza kuwa mmoja wa mapacha wake wachanga amefariki dunia siku ya jana. Chapisho hilo la Ronaldo lilisomeka “Ni kwa masikitiko yetu makubwa tunalazimika kutangaza kwamba mtoto wetu wa kiume ameaga dunia. Ni maumivu makubwa zaidi ambayo wazazi wowote wanaweza kuhisi. Kuzaliwa tu kwa mtoto wetu wa kike kunatupa nguvu ya kuishi wakati huu kwa matumaini na furaha.. Tungependa kuwashukuru madaktari na wauguzi kwa huduma na usaidizi wao wote wa kitaalam. Sote tumehuzunishwa na tunaomba faragha katika wakati huu mgumu sana.. Mtoto wetu wa kiume, wewe ni malaika wetu. Tutakupenda daima.” –Imeeleza taarifa hiyo.

Will Smith Kupigwa Msumari Oscar , Baada Ya Kumshambulia Chris Rock

Waandaji wa Tuzo za #Oscar wamelaani Kitendo kilichofanywa na Muigizaji Will Smith usiku wa Jana katika Ugawaji wa Tuzo hizo. Academy wamesema Kuwa wanafuatilia kwa Ukaribu tukio hilo na Watatoa maamuzi Makali kwa Mujibu wa Sheria zinavyosema. TAZAMA VIDEO YA TUKIO HILO Smith ameingia Kwenye vichwa vya Habari baada ya Kumpiga kibao shavuni Mchekeshaji Chris Rock kwenye Jukwaa la Tuzo hizo Kutokana na Utani wa  Rock kwa Jada Pinkett Smith's ambaye ni Mke wake aliposema Kuwa nywele za Mwanamama huyo ni Mbaya kwa sababu Anaelekea kuwa na Kipara. Pinkett Smith alishawahi Kusema kuwa Ana tatizo Lijulikano kitaalamu Kama Alopecia (Hali ya Kupoteza nywele Kichwani.

Hamisa Mobetto Alamba Dili la Mamilioni , Kukaa Meza Moja Na Blac Chyna

Mwanamitindo na mjasiriamali kutokea nchini Tanzania, Mwanadada Hamisa Mobetto amesaini dili nono la ubalozi wa vipodozi vya Whitenicious kwa upande wa Bara la Afrika akimsaidia mwanadada Blac Chyna kutoka nchini Marekani ambaye ni balozi wa bidhaa hizo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Hamisa ametambulisha Ubalozi huo na kuandika “ Hatimaye siri ya urembo wangu ni hii. Ningependa kutangaza rasmi kwamba nimekuwa balozi wa Whitenicious Afrika. Kwa kushirikiana na Whitenicious nitatangaza urembo kwa kutumia bidhaa za asili kwaajili ya wanaume na wanawake. Kwa miaka mingi Afrika imekuwa ikipokea bidhaa za urembo zenye kemikali. Bidhaa hii inamiaka 30 sokoni ikihakikisha ngozi za wanawake na wanaume zikiwa salama ” - Hamisa Mobetto Mrembo huyu ukiachilia mbali dili hili la vipodozi vya kimataifa, Milango ya kibiashara inazidi kufunguka kwani pia ni balozi wa kinywaji cha Belaire.

Huyu Ndiye Vladimir Vladimirovich Putin

Potrait of A.HP By Heinrich Krirr 1937 Rais wa Urusi, Vladimir Vladimirovich Putin alizaliwa mwaka wa 1952 katika mji wa St. Petersburg (wakati huo ikiitwa Leningrad). Baada ya kuhitimu Chuo Kikuu cha Jimbo la Leningrad, Putin alianza taaluma yake katika shirika la kijasusi la nchi hiyo linalojulikana kama (KGB) katika ngazi ya afisa wa ujasusi mwaka 1975. Putin alipanda vyeo haraka katika Serikali ya hiyo baada ya kujiunga na utawala wa Rais Boris Yeltsin mwaka 1998, na kuwa waziri mkuu mwaka 1999 kabla ya kuwa kiongozi mkuu wa nchi hiyo. Putin aliteuliwa tena kuwa waziri mkuu wa Urusi mwaka 2008, na mwaka 2012 alichaguliwa kuwa Rais wa Urusi. Kufuatia kuanguka kwa Umoja wa Kisovieti mwaka 1991, Vladimir Putin alistaafu kutoka KGB akiwa na cheo cha kanali, na akarudi Leningrad kama mfuasi wa Anatoly Sobchak (1937-2000), mwanasiasa huria. Katika uchaguzi wa mwisho kama Meya wa Leningrad (1991), Putin alikua mkuu wake wa kitengo cha uhusiano wa mambo ya nje na Naibu Meya wa kwanza...

Harmonize Awaondoa Jux , Darassa Afro East Carnival

Mkurugenzi wa lebo ya Konde Music World Wide Harmonize amewaondoa wasanii Jux na Darassa katika orodha ya wasanii watakaotumbuiza kwenye tamasha la Afro East Carnival baada ya wakali hao kudai kuwa hawana makubaliano yoyote Juu ya kuwepo kwao kwenye tamasha hilo ambalo limeandaliwa na Harmonize  litakalo fanyika tarehe 05 March 2022 maeneo ya Tabata Shule. Kupitia Empire ya Efm Jux amesema kuwa yeye binafsi (Jux) alimtafuta Konde Boy na kumuelezea hatua alizozipitia kwenye makubaliano hayo kuwa sio Sahihi lakini hawakuchukulia serious inshu hiyo. Jux ameeleza kuwa , Ni kweli Harmonize aliwahi kumtafuta na kumuelezea kuhusu Afro East Carnival , na baada ya hapo hawakuzungumza lolote kuhusu malipo na ratiba yake , Ila walichokubaliana ni kwamba vitu vikiwa tayari waambiane kwa ajili ya mikataba zaidi , Ila Jux anasema kuwa siku ya leo aliamka na kukuta tangazo limewekwa tayari kuwa atakuwepo kwenye show hiyo. AfricanBoy ameongeza kuwa baada ya kuliona Tangazo , Aliutafuta Uo...

Diamond Platnumz Aweka Rekodi Mpya Africa Mashariki

SIMBA , Diamond Platnumz amejiwekea rekodi nyingine baada kutumbuiza kwenye tamasha maalum lililoandaliwa na waandaaji wa tuzo za Grammy na kumfanya kuwa msanii wa kwanza kutoka ukanda wa Afrika Mashariki kutumbuiza kwenye show hiyo inayokwenda kwa jina la Global Spin Show hii ambayo huwa inaruka mubashara kwa njia ya mtandao kupitia  YouTube , Twitter , Facebook za Recording Academy ilianzishwa mwishoni mwa mwaka 2021 ikiwa na lengo la kuibua na kuutangaza zaidi muziki wa Afro Beat K-Pop na Latin Music Sehemu Ya Show Hiyo Ya Diamond Platnumz  Diamond pia ameutambulisha wimbo wake mpya unaokwenda kwa Jina la Gidi katika show hiyo , Huku akichanganya vionjo  vya wimbo wa Wizkid unaoitwa Show You The Money