Skip to main content

Posts

Zuchu Afikia Rikodi Hii Instagram , Awatibua Mastaa Wa Kike Bongo

Zuhura Othman anayetambulika kwa jina lake la kisanaa kama Zuchu anazidi kupanda nafasi kila kukicha baada ya kufikisha wafuasi milioni 5 katika mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo sasa anakaribia kuwafikia wafuasi wa msanii mwenzake Nandy ambaye ana wafuasi milioni 6.6 katika mtandao huo. Juma lililopita Zuchu alichapisha chapisho katika ukurasa wake wa instagram na kuwataka mashabiki zake kutomfanisha na msanii yoyote wa kike kutokea ukanda wa Afrika Mashariki na kudai kuwa kwa hatua aliyofika anapaswa kupambanishwa na wasanii wa kiume kwani anao uwezo mkubwa wa kuandika nyimbo na kutunga. “ Niwashukuru Wazazi wangu ni kwa ajili yenu na Uwezo wa m/mungu tu .kwa uandishi wangu yafaa kuwekwa kwenye ligi za wanaume wadada wenzangu ntawaonea tu. Respectfully my pen game hard I could write for a guy and not notice. Releasing two songs this month ,” - Zuchu. Zuchu ambaye anatamba na nyimbo zake mbili mpya alizoziachia hivi karibuni " Jaro " na " Fire " ndiye msanii ...

Erik ten Hag Asisitiza kuwa Ronaldo Hauzwi Manchester United

Kocha Mkuu wa Manchester United, Erik Ten Hag amesema mchezaji wa klabu hiyo na taifa la Ureno nyota Cristiano Ronaldo hatouzwa kwa sababu klabu hiyo ina malengo naye kwa ajili ya msimu ujao. Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na tetesi za kuwa Ronaldo anahitaji kuondoka United. Ten Hag ameongeza kuwa “Niliongea na Ronaldo kabla ya haya mambo kujitokeza na maongezi yetu yalikuwa mazuri na niko na mpango naye wa kumtumia tunataka kupate mafanikio tukiwa naye, kama nilivyosema mwanzo Ronaldo hauzwi” Aidha Erik ten Hag amethibitisha kuwa Harry Maguire atasalia kama nahodha wa Manchester United kwa msimu ujao na haoni kumbakiza nahodha kama suala muhimu. Huku United wakimwinda Lisandro Martinez msimu huu wa joto, Maguire atakabiliwa na ushindani zaidi katika nafasi yake na kumekuwa na uvumi kwamba Ten Hag anaweza kuteua nahodha mpya , Lakini Ten Hag amemuunga mkono Maguire kubaki na kitambaa hicho msimu huu. “Harry Maguire ndiye nahodha. Ni lazima niwafahamu wachezaji wote, lakini ni nahod...

Jux Akutana na Boss wa Hennessy , Apewa zawadi Yenye thamani ya EURO 3100

Msanii wa muziki wa RnB Juma Jux kutokea kiwanda cha muziki wa Bongo fleva ameendelea kutanua wigo wa biashara zake Kimataifa ambapo siku ya jana ameingia kwenye headlines kwa mara nyingine baada ya kuchapisha video katika ukurasa wake wa Instagram ikimuonesha akiwa kwenye mualiko wa chakula cha jioni na Boss na mwanafamilia waanzilishi wa Hennessy, bwana Maurice R. Hennessy. Kwenye mualiko huo, Jux pia amepewa zawadi ya chupa ya Hennessy iliyoandikwa jina lake, inayokadiriwa kuwa na thamani ya Euro 3,100 ambazo ni zaidi ya Shillingi Milioni 7.5 kwa fedha za hapa nyumbani. African Boy anameeleza kuwa safari zake nje ya nchi zitakwenda kufungua fursa nyingi za kibiashara kwake na vijana wengi hapa nchini.

Burna boy Aweka Rikodi mpya Africa , Aingiza Dola $7,276,150 kwa Usiku mmoja

Nyota wa muziki kutokea nchini Nigeria African Giant , Burna Boy ameingiza mabilioni ya fedha kutoka kwenye tamasha alilolifanya siku chache zilizopita Madison Square Garden , New York. Damini Ogulu, anayejulikana kwa jina lake la kisanaa kama Burna Boy, amekuwa msanii wa kwanza wa muziki wa Nigeria kufikia rikodi hiyo ambapo Odogwu amejinyakulia zaidi ya bilioni N3 za mauzo ya tiketi pekee. Tiketi ziliuzwa kwa bei ya chini kwa dola $80 na wastani wa dola $350 huku tiketi za juu Zikiuzwa kwa dola $2,125. Kulingana na hesabu za Business Day kwa kutumia wastani wa mauzo ya N145,365.50 ambapo ni dola ($350) ikizidishwa na jumla ya uwezo kuchukua watazamaji unaopatikana katika uwanja wa huo 20,789, na kiwango cha ubadilishaji cha sasa cha fedha za kigeni nchini Nigeria N415.33 jumla yake ni $7,276,150 ambayo ni zaidi ya N3,03022,090. . Tamasha hilo la kihistoria lililotumia takribani saa 2 liliruka moja kwa moja kwenye Youtube na kupata watazamaji zaidi ya 81,000 mashabiki kutoka nc...

Mtoto wa Kiume wa Cristiano Ronaldo Afariki Usiku wa Jana

Mshambuliaji wa Manchester United raia wa Ureno , Cristiano Ronaldo kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii ametangaza kuwa mmoja wa mapacha wake wachanga amefariki dunia siku ya jana. Chapisho hilo la Ronaldo lilisomeka “Ni kwa masikitiko yetu makubwa tunalazimika kutangaza kwamba mtoto wetu wa kiume ameaga dunia. Ni maumivu makubwa zaidi ambayo wazazi wowote wanaweza kuhisi. Kuzaliwa tu kwa mtoto wetu wa kike kunatupa nguvu ya kuishi wakati huu kwa matumaini na furaha.. Tungependa kuwashukuru madaktari na wauguzi kwa huduma na usaidizi wao wote wa kitaalam. Sote tumehuzunishwa na tunaomba faragha katika wakati huu mgumu sana.. Mtoto wetu wa kiume, wewe ni malaika wetu. Tutakupenda daima.” –Imeeleza taarifa hiyo.

Will Smith Kupigwa Msumari Oscar , Baada Ya Kumshambulia Chris Rock

Waandaji wa Tuzo za #Oscar wamelaani Kitendo kilichofanywa na Muigizaji Will Smith usiku wa Jana katika Ugawaji wa Tuzo hizo. Academy wamesema Kuwa wanafuatilia kwa Ukaribu tukio hilo na Watatoa maamuzi Makali kwa Mujibu wa Sheria zinavyosema. TAZAMA VIDEO YA TUKIO HILO Smith ameingia Kwenye vichwa vya Habari baada ya Kumpiga kibao shavuni Mchekeshaji Chris Rock kwenye Jukwaa la Tuzo hizo Kutokana na Utani wa  Rock kwa Jada Pinkett Smith's ambaye ni Mke wake aliposema Kuwa nywele za Mwanamama huyo ni Mbaya kwa sababu Anaelekea kuwa na Kipara. Pinkett Smith alishawahi Kusema kuwa Ana tatizo Lijulikano kitaalamu Kama Alopecia (Hali ya Kupoteza nywele Kichwani.

Hamisa Mobetto Alamba Dili la Mamilioni , Kukaa Meza Moja Na Blac Chyna

Mwanamitindo na mjasiriamali kutokea nchini Tanzania, Mwanadada Hamisa Mobetto amesaini dili nono la ubalozi wa vipodozi vya Whitenicious kwa upande wa Bara la Afrika akimsaidia mwanadada Blac Chyna kutoka nchini Marekani ambaye ni balozi wa bidhaa hizo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Hamisa ametambulisha Ubalozi huo na kuandika “ Hatimaye siri ya urembo wangu ni hii. Ningependa kutangaza rasmi kwamba nimekuwa balozi wa Whitenicious Afrika. Kwa kushirikiana na Whitenicious nitatangaza urembo kwa kutumia bidhaa za asili kwaajili ya wanaume na wanawake. Kwa miaka mingi Afrika imekuwa ikipokea bidhaa za urembo zenye kemikali. Bidhaa hii inamiaka 30 sokoni ikihakikisha ngozi za wanawake na wanaume zikiwa salama ” - Hamisa Mobetto Mrembo huyu ukiachilia mbali dili hili la vipodozi vya kimataifa, Milango ya kibiashara inazidi kufunguka kwani pia ni balozi wa kinywaji cha Belaire.

Huyu Ndiye Vladimir Vladimirovich Putin

Potrait of A.HP By Heinrich Krirr 1937 Rais wa Urusi, Vladimir Vladimirovich Putin alizaliwa mwaka wa 1952 katika mji wa St. Petersburg (wakati huo ikiitwa Leningrad). Baada ya kuhitimu Chuo Kikuu cha Jimbo la Leningrad, Putin alianza taaluma yake katika shirika la kijasusi la nchi hiyo linalojulikana kama (KGB) katika ngazi ya afisa wa ujasusi mwaka 1975. Putin alipanda vyeo haraka katika Serikali ya hiyo baada ya kujiunga na utawala wa Rais Boris Yeltsin mwaka 1998, na kuwa waziri mkuu mwaka 1999 kabla ya kuwa kiongozi mkuu wa nchi hiyo. Putin aliteuliwa tena kuwa waziri mkuu wa Urusi mwaka 2008, na mwaka 2012 alichaguliwa kuwa Rais wa Urusi. Kufuatia kuanguka kwa Umoja wa Kisovieti mwaka 1991, Vladimir Putin alistaafu kutoka KGB akiwa na cheo cha kanali, na akarudi Leningrad kama mfuasi wa Anatoly Sobchak (1937-2000), mwanasiasa huria. Katika uchaguzi wa mwisho kama Meya wa Leningrad (1991), Putin alikua mkuu wake wa kitengo cha uhusiano wa mambo ya nje na Naibu Meya wa kwanza...

Harmonize Awaondoa Jux , Darassa Afro East Carnival

Mkurugenzi wa lebo ya Konde Music World Wide Harmonize amewaondoa wasanii Jux na Darassa katika orodha ya wasanii watakaotumbuiza kwenye tamasha la Afro East Carnival baada ya wakali hao kudai kuwa hawana makubaliano yoyote Juu ya kuwepo kwao kwenye tamasha hilo ambalo limeandaliwa na Harmonize  litakalo fanyika tarehe 05 March 2022 maeneo ya Tabata Shule. Kupitia Empire ya Efm Jux amesema kuwa yeye binafsi (Jux) alimtafuta Konde Boy na kumuelezea hatua alizozipitia kwenye makubaliano hayo kuwa sio Sahihi lakini hawakuchukulia serious inshu hiyo. Jux ameeleza kuwa , Ni kweli Harmonize aliwahi kumtafuta na kumuelezea kuhusu Afro East Carnival , na baada ya hapo hawakuzungumza lolote kuhusu malipo na ratiba yake , Ila walichokubaliana ni kwamba vitu vikiwa tayari waambiane kwa ajili ya mikataba zaidi , Ila Jux anasema kuwa siku ya leo aliamka na kukuta tangazo limewekwa tayari kuwa atakuwepo kwenye show hiyo. AfricanBoy ameongeza kuwa baada ya kuliona Tangazo , Aliutafuta Uo...

Diamond Platnumz Aweka Rekodi Mpya Africa Mashariki

SIMBA , Diamond Platnumz amejiwekea rekodi nyingine baada kutumbuiza kwenye tamasha maalum lililoandaliwa na waandaaji wa tuzo za Grammy na kumfanya kuwa msanii wa kwanza kutoka ukanda wa Afrika Mashariki kutumbuiza kwenye show hiyo inayokwenda kwa jina la Global Spin Show hii ambayo huwa inaruka mubashara kwa njia ya mtandao kupitia  YouTube , Twitter , Facebook za Recording Academy ilianzishwa mwishoni mwa mwaka 2021 ikiwa na lengo la kuibua na kuutangaza zaidi muziki wa Afro Beat K-Pop na Latin Music Sehemu Ya Show Hiyo Ya Diamond Platnumz  Diamond pia ameutambulisha wimbo wake mpya unaokwenda kwa Jina la Gidi katika show hiyo , Huku akichanganya vionjo  vya wimbo wa Wizkid unaoitwa Show You The Money

Otile Brown Athibitisha Kutengana Na Mpenzi Wake Muethiopia

Mwanamuziki kutokea nchini Kenya Otile Brown amethibitihsa kuachana na mpenzi wake anayejulikana kwa Jina Nabbayet raia wa Ethiopia. Otile ameweka wazi hayo kupitia Insta story yake kwa Kuandika kuwa mara ya mwisho kuwasiliana na Nabbi walijaribu kusuluhisha changamoto walizokuwa wakizipitia lakini haikuwezekana hivyo kila mtu akaamua aendelee na maisha yake. Otile ameandika “Mimi na Nabbi hatuko pamoja tena, mara ya mwisho kuwa nae tulikuwa tunajaribu kutatua changamoto zetu lakini tukalidhia kutengana.” Hata hivyo licha ya kutengana huko Otile amesema kuwa “Nabbi ni mtu mwema sana , nitaendelea kumuheshimu , kumjali na kuwa na amani kati yetu. Namtakia maisha mema”

Harmonize Atangaza Kuhamia Kwenye Filamu

Mkurugenzi wa lebo ya Konde Music Worldwide Harmonize ametangaza kuingia kwenye fani ya uigizaji wa filamu muda wowote kuanzia sasa. Kondeboy ameweka wazi hilo kupitia Insta Story yake ambapo amebainisha kuwa filamu hiyo kwa mara ya kwanza itaoneshwa kupitia mtandao wa Ceek , Kampuni ambayo inajihusisha na masuala ya burudani kama kurusha matukio ya mubashara mtandaoni, kuandaa matamasha, kutengeneza headphones n.k Harmonize ameandika “Nimechoka kusubiri filamu yangu ya kwanza. Itakuwa kali sana, tukutane Ceek hivi karibuni jisajili sasa” - Harmonize

Diamond Platnumz Atua Nigeria Kimya Kimya , Akutana Na Jay Willz

  Jay Willz akiwa Na Diamond Platnumz Mwaka 2022 umeanza kwa kasi sana kwa mwanamuziki  Diamond Platnumz kutokana na kazi zake za Muziki , Baada ya kumaliza kolabo na The Ben kutoka nchini Rwanda Diamond sasa Amevuka mipaka mpaka nchini Nigeria. Nyota huyo ambaye ni mkurugenzi wa lebo ya muziki WCB Wasafi kwa sasa Yupo nchini Nigeria akiwa anakamilisha video na msanii wa muziki kutokea nchini humo anayeitwa  Jay Willz  ambaye anatamba na wimbo wake unaoitwa Medicine aliouachia tangu Agost 25, 2021. Kupitia ukurasa wake wa katika mtandao wa Instagram Jay Willz amechapisha picha akiwa na Diamond katika moja ya Eneo ambalo wanatayarisha  video Hiyo na kuambatanisha maneno yaliyosomeka “ Diamond Platnumz feat Rolly Boy Big 2022 ” Diamond Platnumz ametua Nchini humo kimya kimya  kukamilisha kideo hicho na Huku akiwa na shughuli zingine za kimuziki katika taifa hilo.

John Cena Achukua Nafasi ya Finn Balor , Sasa Kupambana Na Roman Reigns Agosti 21

Mkongwe wa WWE John Cena usiku wa Jana alirejea tena Kwenye kampuni hiyo Baada ya kukaa Nje ya mchezo Huo kwa Muda wa mwaka mmoja na nusu , Kurudi kwake kumeifanya WWE kurejea kwa Kishindo huku John akikiri kwamba Amerejea katika Mchezo huo kuuchukua Utawala wa Mashindano hayo Makubwa nchini Marekani. Baada ya tukio hilo Sasa Bingwa wa WWE Universal Champion Roman Reigns atakabiliana na John Cena hii ni baada ya John kusaini mkataba wa Kupambana na Mpinzani huyo mnamo Agosti 21. Awali Roman Reigns aligoma Kupigana na John Cena kwenye kipindi cha Smack Down wiki iliyopita na  kukubali kupambana na Mpinzani mwingine Finn Balor kisha John Cena akatokea na Kuchukua nafasi ya Finn hivyo Mpambano rasmi utakuwa Agosti 21 mwaka 2021.

Kanye West Atunukiwa Heshima Katika Jiji la Atlanta ' Julai 22 Yatajwa Kuwa Siku Ya KANYE WEST

Masaa machache Kabla ya Kanye West kuingia Jukwaani Katika Uzinduzi wa albamu ya DONDA, Rapa huyo alijikuta Akipokea heshima kutoka kwa uongozi wa Jiji la Atlanta kwa kumtunuku siku ya tarehe 22, Julai kila Mwaka katika jiji hilo kuwa siku ya KANYE WEST. Katika Uzinduzi wa Awali wa albamu hiyo Usiku wa Jana ' Wakaazi wa Jiji la Atlanta walifanikiwa Kuujaza uwanja wa Mercedes Benz kwa Lengo la kuisikiliza Albamu ya DONDA huku Kwa mara ya Kwanza baada ya Kitambo rapa Jay Z atasikika tena Katika moja ya Nyimbo zinazopatikana Katika albamu hiyo ' Pia mwanamama Kim Kardashian akiwa Ameongozana na Watoto wake North , Saint , Chicago , and Psalm walikuwepo Katika kuisikiliza Albamu hiyo. Kanye West alizaliwa huko Atlanta na aliishi Katika jiji hilo hadi Alipokuwa na miaka Mitatu kufuatia wazazi wake Kuachana.  Baba yake anaitwa Ray West, alikuwa mwandishi wa picha na Jarida la Atlanta na Mama yake, marehemu anaitwa Donda West, alikuwa Profesa wa Kiingereza katika Chuo Kikuu cha Clark ...

Leo Messi Kusaini Mkataba Mpya Barcelona Mpaka Mwaka 2026

 Rasmi sasa Klabu ya Barcelona Ina uhakika Asilimia 100 kumbakisha mchezaji Tagemezi wa klabu hiyo Leo Messi kwa kuwa Mshambuliaji huyo Yupo mbioni kusaini mkataba Mpya na Wanacatalunya hao ' Mkataba utakao mbakisha Uhispania mpaka Mwaka 2026. Habari za kuaminika Kutoka ndani ya Klabu zinasema kuwa Tayari makubaliano ya Awali kuhusu mkataba mpya Yalishafanyika hivyo Vimebakia vitu vichache na Rasmi watatoa tamko siku Chache zijazo. Mwanzo Messi alitaka Kusaini miaka 3 Kuitumikia miamba hiyo Ila sasa atasaini Miaka 5 itakayomweka Fc Barcelona mpaka mwaka 2026 huku akikubali Kupunguza mshahara Wake.

Diamond Platnumz Akutana na Snoop Dog Marekani

Nyota wa Bongofleva Diamond Platnumz Bado yupo nchini Marekani akiwa Katika Maandalizi ya Mwisho ya Album yake Ambayo Itatoka siku za Hivi karibuni. Akiwa nchini Humo Diamond Platnumz ameshakutana na Wasanii wengi Wakubwa na Siku ya Jana Alifanikiwa kukutana na Mkali wa Muziki wa Kufoka Legendari Snoop Dogg. Katika video Hii  Snoop Dog amemueleza diamond platnumz ni Kwa kiasi Gani Jamii yake Ya karibu Ilivyomkataa Kipindi Anaanza Muziki ' Mpaka sasa kufikia kuwa Mfano wa Kuigwa  na Wasanii wengine Chipukizi na Waliopo kwenye Muziki. TAZAMA MAZUNGUMZO YA DIAMOND NA SNOOP DOG

Sergio Ramos Afunguka Mwanzo Mwisho Sababu za Kuondoka Real Madrid

Klabu ya Real Madrid imethibitisha kuwa nahodha wake Sergio Ramos ataondoka klabuni hapo katika dirisha la usajili la majira ya joto (Summer) baada ya kuhudumu klabuni hapo kwa miaka 16. Awali Madrid walituma ofa ya mwaka mmoja huku nyota huyo akitaka angalau mkataba wa miaka miwili. Rais wa Real Madrid, Florentino Perez ameweka wazi kuwa, wakati makubaliano ya mkataba mpya na Ramos hayakufikiwa na kusisitiza kuwa Sergio Ramos ataendelea kukaribishwa tena klabuni hapo kwa siku za usoni. Katika sherehe za kumuaga Sergio Ramos zilizofanyika Madrid siku ya jana. Ramos amefunguka ukweli wote ikiwemo taarifa ya kuomba apewe mkataba mpya tangu 2018 baada ya fainali za michuano ya UEFA mwaka huo , Lakini Perez alikuwa akitoa ahadi hewa. Unaambiwa katika zama za Perez hakuna Legend aliyestaafu akiwa na jezi ya Real Madrid. MKUTANO WA SERGIO RAMOS NA WAANDISHI WA HABARI Real Madrid walitaka kunipa mkataba mpya nami nilikubaliana nao, ukiwa na kipengele cha kupunguza mshahara kwa 10% , Sikuwa na...

Diamond Platnumz Awakimbiza Wizkid , Burna Boy Tuzo za BET

Nyota wa muziki kutokea nchini Tanzania, Naseeb Abdul Juma maarufu kwa jina Diamond Platnumz ameonekana kupata muitikio mkubwa kwenye post za wasanii wa Afrika aliokutana nao kwenye kipengele cha "Best International Act" kwenye tuzo za BET 2021. Diamond amepata muitikio wa idadi kubwa ya maoni na 'likes' kwenye post za Instagram za wiki iliyopita za ukurasa wa 'Bet Africa' tofauti na wasanii wengine wa Afrika aliokutanishwa nao kwenye kipengele hicho cha tuzo. Diamond akiwa ni msanii pakee kutokea Afrika Mashariki kuteuliwa kuwania tuzo hizo, wasanii aliokutanishwa nao kutoka Afrika ni pamoja Burnaboy, Wizkid. Kwenye kupengele hicho cha 'Best International Act', Diamond Platnumz mbali na Diamond  kukutana na wasanii hao kutokea nchini Nigeria pia amekutanishwa na Aya Nakamura (France), Emicida (Brazil), Headie One (Uk), Young T & Bugsey (Uk) na Youssoupha (France). Hii ndiyo Orodha ya Wasanii Wanao Wania Tuzo hii Na Diamond Platnumz Hata...